Entertainment
Davido Amzawadi Mkewe Chioma Mamilioni ya Fedha Wakati wa Harusi ya Kifahari ‘White Wedding’ Huko Miami

Davido, mmoja wa wanamuziki wakubwa wa Nigeria, ameonesha wazi kwamba furaha na mapenzi kwake hayawekewi kikomo cha fedha. Usiku wa kuamkia leo, msanii huyo alishangaza na kufurahisha mashabiki baada ya kumzawadia mke wake mpendwa, Chioma, saa ya kifahari aina ya Richard Mille yenye thamani ya takribani dola 300,000 – sawa na zaidi ya Ksh milioni 38.76 au Naira milioni 465 kwa thamani ya nchini kwao.
Hii si zawadi ya kawaida, bali ni sehemu ya msururu wa zawadi na matukio ya kifahari ambayo Davido ameandaa kwa mke wake katika sherehe yao ya White Wedding inayoendelea mjini Miami, Marekani. Sherehe hii, inayotajwa kuwa miongoni mwa harusi za kifahari zaidi barani Afrika, inakadiriwa kugharimu takriban dola milioni 3.7 – sawa na zaidi ya bilioni 477 za kikenya.
Kwa mashabiki wa Davido, msemo maarufu “Chioma ni Davido na Davido ni Chioma” unapata maana halisi. Ni taswira ya upendo wa kweli uliojengwa kwa heshima, uaminifu, na furaha tele. Wawili hawa wamekuwa mfano wa wanandoa wanaoshirikiana katika kila hatua ya maisha, wakiishi hadharani bila kuogopa kuonyesha hisia zao.
Sherehe hii ya kifahari imekusanya wageni mashuhuri kutoka pembe zote za dunia, huku muziki, vicheko, na mitindo ya hali ya juu vikijaza anga ya Miami. Davido, anayejulikana kwa ukarimu wake wa kipekee, ameendelea kuthibitisha kwamba maisha ni ya kuishi kwa furaha na kusherehekea wale unaowapenda bila kujali gharama.
Kwa wapenzi wa habari na burudani, unaweza kufuatilia matukio haya mubashara kupitia COCO FM kwenye 98.9 FM, kupitia WWW.COCOMEDIA.CO.KE na Radio Garden ukitafuta COCO FM, au kutazama moja kwa moja kupitia YouTube channel ya COCO FM RADIO.
Entertainment
Mboga Imejileta; Arrow Bwoy Aitisha Pigano Dhidi ya Shakib

Msanii maarufu wa Kenya, Arrow Bwoy, amezua gumzo mtandaoni baada ya kumualika wazi wazi mfanyabiashara kutoka Uganda, Shakib Cham, kwenye pambano la ndondi.
Hii imekuja baada ya kipigo cha hadharani ambacho Shakib alipokea kutoka kwa msanii mwenzake wa Uganda, Rickman, hali iliyoacha mashabiki wengi wakisema: “Sasa ata Arrow Bwoy anaweza!”
Kupitia video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Arrow Bwoy, anayefahamika kwa vibao kama Digi Digi, hakuonyesha woga wowote. Kwa ucheshi, alisema amekuwa akisubiri nafasi kama hii kwa muda mrefu.
“Mboga imejileta,” alisema kwa kujiamini, akimaanisha kuwa Shakib amejileta mwenyewe kwenye kipigo.
“Chakula kiko tayari. Niko tayari kwa pambano hili.”
Arrow Bwoy pia hakusita kumtaja mke wa Shakib, Zari Hassan, akimtaka akae mbali na ulingo siku ya pambano hilo kwa usalama wake binafsi.
“Zari, usijisumbue kuja. Hii si sehemu ya wanawake. Usije ukazimia tukapata janga la pili,” alisema kwa kejeli.
Hata hivyo, wakosoaji wake walikumbusha jamii kuhusu video za awali zinazoonyesha Arrow Bwoy akichapwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Swali likabaki: Je, kweli ana uwezo wa kumpiga Shakib au ni porojo za mitandaoni?
Kwa jina la Zari kuingizwa kwenye sakata hili, mvutano umeongezeka na mashabiki kote Afrika Mashariki wanasubiri kuona kama Shakib atakubali changamoto hii ya kihistoria.
“Zari, kama unasikia, mtume tu kijana wako aje achukue kichapo — kichapo cha kimataifa,” Arrow Bwoy alimalizia kwa msisitizo.
Kwa sasa, macho yote yako kwa Shakib. Je, atakubali changamoto hii na kuweka historia mpya ya burudani Afrika Mashariki?
Entertainment
#CHAN2024: Savara, Zuchu na Eddy Kenzo Kutumbuiza Fainali ya CHAN 2024 Nairobi

Mashindano ya CHAN 2024 yakielekea ukingoni, mashabiki wanatarajiwa kupata burudani ya aina yake kutoka kwa baadhi ya nyota wakubwa wa muziki Afrika Mashariki.
Kenya, Uganda na Tanzania zitawakilishwa vilivyo kupitia majina makubwa matatu: Savara wa Kenya (mwanachama wa zamani wa kundi maarufu Sauti Sol), Eddy Kenzo wa Uganda, na Zuchu kutoka Tanzania, anayejulikana kwa jina halisi Zuhura Othman.
Onyesho hili la kufunga pazia litafanyika sambamba na mechi ya fainali Jumamosi, likitarajiwa kuhamasisha na kuburudisha maelfu ya mashabiki watakaofurika uwanja wa Kasarani. Shoo hiyo inalenga kumaliza mashindano haya ya kihistoria kwa upekee na kiwango cha juu cha burudani.
Mbali na kusubiriwa kwa hamu jukwaani, Savara pia amekuwa na mchango mkubwa nyuma ya pazia. Yeye ndiye mtunzi na mtayarishaji wa wimbo rasmi wa CHAN 2024 unaoitwa “Pamoja”.
Wimbo huo unashirikisha nyota kutoka kanda hii: Elijah Kitaka wa Uganda na Phina wa Tanzania. Uliimbwa kwa mara ya kwanza katika sherehe za ufunguzi na uliweka ladha na hamasa ya mashindano haya.
Ingawa wenyeji wa mashindano haya—Kenya, Uganda na Tanzania—waliishia katika hatua ya robo fainali, fainali za mwaka huu zinaahidi kuwa kilele cha msisimko.
Burudani kutoka kwa Zuchu, Savara na Eddy Kenzo itakuwa chachu ya kuhitimisha mashindano yaliyojaa matukio na hisia.
Kwa upande mwingine, kumekuwa na malumbano mitandaoni kati ya mashabiki wa Kenya na Tanzania, hususan baada ya timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, kudondoshwa nje ya michuano hiyo katika robo fainali.
Mashabiki wa Tanzania hawakusita kuchokoza wenzao kwa kejeli, jambo lililoongeza ladha ya ushindani wa nje ya uwanja.