Connect with us

Entertainment

Christina Shusho Azua Gumzo Baada ya Kumsifia Rais Samia

Published

on

Msanii maarufu wa muziki wa Injili kutoka Tanzania, Christina Shusho, amezua mjadala mkali mitandaoni baada ya kumpongeza hadharani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Hatua hii imewakera baadhi ya mashabiki wake ambao walionesha wazi kutoridhishwa na ujumbe huo.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Shusho alichapisha picha rasmi ya Rais Samia, akifuatisha na maneno ya maombi:

“Neema ya Mungu ikutoshe mama, tunamtukuza Mungu kwa ajili yako.”

Aliendelea kwa kuandika:
“Fanya kwa uwezo wako wa kibinadamu, Mungu atafanya yaliyosalia. Wewe ni fahari yetu, Amina.”

Ingawa ujumbe huo ulionekana wa heshima na maombi, wengi walitafsiri kama kumsifu Rais bila kuzingatia changamoto mbalimbali za kijamii na kisiasa zinazolikabili eneo la Afrika Mashariki, hususan Tanzania na Kenya.

Sehemu ya mashabiki wake walihoji uamuzi wake wa kutoa tamko hilo, huku baadhi wakifurika kwenye sehemu ya maoni wakieleza hasira zao.
Mmoja aliandika kwa ukakasi:

“Unfollow Shusho button.”

Wengine walienda mbali zaidi na kutaka afungwe au kupuuzwa kabisa, wakidai amepuuza hali halisi ya wananchi wa kawaida.

Wachambuzi wa mitandao wanaona kuwa kundi kubwa la wafuasi wake kutoka Kenya pia walihisi kusalitiwa, hasa kwa kuzingatia muktadha wa hivi karibuni wa kisiasa na kijamii unaohusisha nchi hizo mbili.

Hali hii inaibua swali pana kuhusu nafasi ya wasanii maarufu katika kujieleza kisiasa—je, wana uhuru wa kuunga mkono viongozi bila kuhukumiwa, au wanapaswa kuwa sauti ya umma kwa kuzingatia hali halisi?

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Steven Otieno: Niliweka Video ya Kujiua WhatsApp – Ilibadilisha Maisha Yangu

Published

on

Katika eneo la Mnarani, Kaunti ya Kilifi, mwanaharakati wa mazingira Stephen Otieno anasimama kama ishara ya ushindi dhidi ya changamoto za maisha. Ni hadithi ya maumivu, kimya, msongo wa mawazo – lakini pia ni simulizi ya matumaini, uponyaji, na kuibuka upya.

Kwenye mahojiano ya kusisimua katika kipindi cha Janjaruka 254, Otieno, amefungua moyo wake kwa mara ya kwanza hadharani kuhusu kipindi kigumu zaidi maishani mwake – alipokaribia kujitoa uhai.

Mizigo ya Matumaini Yasiyolingana na Uhalisia
Baada ya kumaliza masomo, wazazi wa Otieno walikuwa na matarajio makubwa kutoka kwake. Walitarajia msaada wa kifedha, msaada wa kijamii – na hata matumaini ya mafanikio ya haraka. Lakini maisha halisi yalikuwa tofauti. Kipato chake kilikuwa cha ulinzi wa usiku – kazi maarufu kama “askari gongo” – yenye malipo duni na mazingira magumu.

Wazazi wake hawakuweza kuelewa hali hiyo. Walizidi kumlilia msaada bila kufahamu kuwa hata yeye alikuwa akihangaika kuendesha maisha yake na ya mke wake, ambaye alimwoa muda mfupi baada ya kuhitimu masomo. Hilo liliwafanya wazazi wake kuchanganyikiwa zaidi – na hilo ndilo lilikuwa chanzo kikuu cha msongo wa mawazo kwa kijana huyu.

Kimya Kilichokaribia Kugharimu Maisha
Kosa kubwa ambalo Otieno anakiri ni kutoongea. Hakumweleza mtu yeyote kuhusu msukosuko huo – hata mkewe. Alibeba msalaba huo kimya kimya hadi usiku mmoja, akiwa kazini kwenye eneo lisilo na watu wengi, alipoamua kujitoa uhai. Kabla ya kuchukua hatua hiyo ya mwisho, alirekodi video na kuiweka kwenye WhatsApp status yake na kushiriki kwenye kundi moja la marafiki.

Simu zaidi ya 100 ziliingia kwa haraka – watu waliotaka kujua tatizo na kumrai asikate uhai wake. Video ile ya sekunde chache ilibadili kila kitu.

Mwanzo wa Safari ya Uponyaji
Msimamizi wake kazini alikimbia hadi eneo alilokuwepo Steven usiku huo. Ndipo Steven alipomwaga moyo wake – kwa mara ya kwanza – na kueleza hali halisi aliyokuwa nayo. Hilo ndilo lilikuwa chimbuko la safari yake mpya.

Kikao cha familia kilifanyika. Wachungaji walihusishwa. Wataalamu wa afya ya akili walimsaidia. Na kwa mara ya kwanza, jamii ilimskia – na kumwelewa. Aliambiwa kwamba hakustahili kupambana peke yake. Aliambiwa kwamba alihitaji kuongea.

Kugeuka na Kuwa Mchochezi wa Mabadiliko
Kupitia shirika la Baha Madzo Gadze for Charity, Otieno alipata nafasi ya kujitolea katika shughuli za kulinda mazingira. Alipewa majukumu madogo madogo ambayo baadaye yalikuza nafasi yake hadi kuwa Naibu Mwenyekiti, kisha Mwenyekiti wa kikundi hicho. Hapo ndipo aligundua maana ya kweli ya maisha – ya kuwa msaada kwa wengine na kwa mazingira yanayotuzunguka.

Anasema: “Sijafikia malengo yangu kikamilifu, lakini nipo kati ya asilimia 40 hadi 50. Hilo ni jambo kubwa kwa mtu aliyekaribia kujiua. Sasa naona mwangaza.”

Ujumbe kwa Wengine
Steven Otieno amebeba ujumbe mzito kwa vijana na watu wote wanaopitia msongo wa mawazo:

”Ongea na mtu. Hata kama ni mtu wa barabarani. Pigia simu mtu unayemwamini. Post kwa mitandao ya kijamii kama huna wa kuongea naye. Usijifiche. Tangamana. Utajifunza na kusaidiwa.”

Anamalizia kwa kusema:

“Bado naihifadhi ile video niliyorekodi nikitaka kujiua. Sijatamani kuifuta kwenye hifadhi zangu. Sio kwa sababu naifurahia, bali kwa sababu ni kumbukumbu ya wapi nimetoka. Leo hii, nipo hapa kwa sababu niliongea. Na nitaendelea kuzungumza ili wengine waone kuwa kuna tumaini.”

Katika ulimwengu ambapo matarajio ya jamii yanaweza kuvunja nafsi, hadithi ya Stephen Otieno ni ushuhuda wa nguvu ya mazungumzo, msaada wa kijamii, na kuamini kuwa maisha yana thamani – hata unapohisi umekwama. Leo hii, sio tu kuwa amepona, bali amegeuka kuwa sauti ya mabadiliko – kwa binadamu na mazingira.

Continue Reading

Entertainment

Verse Smart, Rojo Mo Amsifia Nyota Ndogo

Published

on

Wimbo mpya wa “BARAKA” unaowakutanisha Rojo Mo, Nyota Ndogo, Chikuzee, na Cannibal The Chosen One unaendelea kumwagiwa sifa kwenye mitandao ya kijamii kwa kukutanisha lejendari wa mziki wa Pwani – si tu kwa beat kali na ujumbe wake wa kusifu Mungu.

Tukio la hivi punde ni Rojo Mo kusifia verse ya Nyota Ndogo kwenye wimbo huo. Rojo Mo, mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa katika scene ya muziki, alitoa maneno haya kupitia ukurasa wake wa Facebook:

“Leo ni NYOTA NDOGO Big up kwa verse smart 🌸 Maua yako pokea #BARAKA”

👉 Tazama video ya BARAKA

Rojo Mo amekuwa akiachia picha za walioshirikiana kwenye wimbo akiskuma link ya wimbo wao; alianza na Chikuzee na sasa amefika kwa Nyota Ndogo. bila shaka kesho tutaona picha ya Canibal aliyemtakia heri kwenye siku ya kuzaliwa Juni tarehe tatu.

Katika wimbo huu, Nyota Ndogo anaingia akisifia penzi analolipata kutoka kwa Mungu kabla ya Chikuzee kuchukua hatamu. Ushirikiano wa wasanii hawa wanne – Rojo Mo nyota wa hits, Nyota Ndogo mkwasi wa sauti kutoka Mombasa, Chikuzee mwenye uandishi wa kina na sauti ya kipekee, pamoja na Cannibal The Chosen One, mkali wa mtindo huru (freestyle) – umeleta ladha ya kipekee kwenye track hii.

Kando na ubunifu wa kisanaa, wimbo wa BARAKA unajitokeza pia kama aina ya wimbo wa kusifu na kutoa shukrani – sio kwa mtazamo wa kidini pekee, bali wa maisha ya kila siku. Wasanii wote wanne wanaelezea jinsi Mungu anavyowafungulia milango ya baraka na ufanisi. Wanarejesha sifa kwa Mungu kwa matendo yake makuu.  Maneno yao yanagusa roho na kutufundisha kuwa kila hatua ya maendeleo si tu baraka inayostahili kusherehekewa bali pia ni fursa ya kumpa Mungu shukurani.

Huu ni wimbo unaotufundisha kuona uzuri hata katika magumu, na kukumbuka kusema “asante” – kwa uhai, kwa familia, kwa kipaji, na hata kwa yale tuliyoyapitia. Kwa namna ya kipekee, BARAKA inakuwa sauti ya sifa, sala ya mitaani, na salaam ya matumaini kwa yeyote anayeisikiliza akiwa kwenye safari yake ya maisha.

Mashabiki mitandaoni wameonyesha mapenzi yao kwa wimbo huu, wakisifia utunzi, video ya kuvutia, na “chemistry” ya wasanii waliokutana. Lakini zaidi.

Katika dunia ya muziki, si kila wimbo ni wa kawaida. Wimbo wa “BARAKA” ni reminder kwamba muziki unaweza kuwa tiba, kuwa nuru, na kuwa silaha.

Continue Reading

Trending