Connect with us

Sports

Chipolpolo Ya Zambia Inazidi Kujinoa Kambini Lusaka Tayari Kwa Chan

Published

on

SIKU 11 ZIMESALIA KWA KOMBE LA CHAN KUNGOA NANGA

ZAMBIA- Chipolopolo

Hii leo tunangazia Taifa la Zambia,wanajiita Chipolopolo kwa jina la Utani,ikiwa inaorodheshwa nafasi ya 87 kote ulimwenguni na Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA.

Kocha mkuu wa Kikosi hicho ni Avram Grant raia wa taifa la Israel, hata hivyo kwenye kipute cha Chan vijana hao wataongozwa na kocha wa nyumbani na mshambulizi wa zamani wa Nchanga Rangers na Power Dynamos Wedson Nyirenda.

Chipolopolo wameshiriki kombe hilo mara nne (2009, 2016, 2018, 2020) ila wameambulia patupu bila kushinda wakimaliza ya tatu katika mwaka wa kwanza wa kombe hilo mwaka 2009 nchini DR.Congo.

Timu hiyo ni mabingwa mara moja taji la AFCON wakishinda mwaka 2012 na pia ni mabingwa mara saba kombe la COSAFA ukanda wa Afrika Kusini.

Timu hiyo yenye wachezaji 32 itaongozwa na nahodha na mzee wa kazi beki wa zamani wa TP Mazembe  Kabaso Chongo ambaye kwa sasa anapiga na Kabwe Worriors ya taifa hilo.

Badhi ya nyota wengine wa kuangaziwa katika kikosi hicho ni pamoja na mshambulizi Joseph Phiri na Evans Kayombo;

GOALKEEPERS); Francis Mwansa (Zanaco), Willard Mwanza (Power Dynamos), Levison Banda (Zesco United), Charles Kalumba (Red Arrows).

(DEFENDERS); Benedict Chepeshi, Kabaso Chongo (all Zesco United), Mathews Banda, Kendrick Mumba, (both Nkana), Killian Kanguluma (Kabwe Warriors), Kebson Kamanga, Happy Nsiku (all Red Arrows), Lyson Banda (Green Buffaloes), Dominic Chanda (Power Dynamos), John Chishimba (Zanaco).

(MIDFIELDERS); Owen Tembo, Frederick Mulambia, Prince Mumba (both Power Dynamos), Kelvin Kapumbu (Konkola Blades), Wilson Chisala (both Zanaco), Philimon Chilimina (both Green Buffaloes), Rally Bwalya (Napsa Stars), Abraham Siankombo, Kelvin Kampamba (both Zesco United), Jackson Kampamba (Mutondo Stars), Kenneth Kasanga (Nkwazi), Timothy Sichalwe (Athletico), Kelvin Mwanza (Muza FC).

(STRIKERS); Andrew Phiri (MUZA), Evans Kayombo (Napsa Stars), Charles Zulu (Nkana), Joseph Phiri (Red Arrows), Kenan Phiri (Makeni All Stars).

Zambia wako kundi A pamoja na Kenya,Angola,Morocco na Dr. Congo

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Published

on

By

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.

WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.

Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.

Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:

  • Urusi

  • Sri Lanka

  • Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota

  • Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)

Continue Reading

Sports

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Published

on

By

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.

Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.

Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.

Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.

Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.

“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”

Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.

Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.

Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.

Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.

Continue Reading

Trending