Connect with us

Entertainment

Chameleone Aongelea Madai Kuhusu Kufungwa Gerezani, Afichua Anafanyiwa Upasuaji

Published

on

Msanii maarufu wa Uganda, Jose Chameleone, amekanusha vikali uvumi unaodai kuwa amefungwa gerezani, akibainisha kuwa yuko hospitalini kwa ajili ya upasuaji muhimu.

Haya yanajiri baada ya video ya mwanadada akidai kwamba msanii huyo amefungwa gerezani kusambazwa mitandaoni.

Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii siku ya Jumanne jioni, Chameleone, ambaye jina lake halisi ni Joseph Mayanja, aliwashukuru mashabiki wake kwa upendo na maombi yao wakati wa kipindi kigumu anachopitia.

Pia alieleza kusikitishwa na video inayosambaa ikidai kuwa amefungwa, akisema:

“Ninawashukuru nyote kwa upendo na maombi yenu. Nimeona video ya mwanadada mmoja mdogo akisema uongo kuhusu mimi kuwa jela n.k. Watu wa aina hiyo wana mawazo gani, hata hivyo? Niko hapa kwa ajili ya upasuaji wangu na nitawajulisha maendeleo yangu. Asanteni watu wangu,” Chameleone alisema.

Aliambatanisha ujumbe wake na video iliyomuonyesha akiongea huku akiwa amelala katika kitanda cha hospitali.

Chameleone amekuwa akipambana na matatizo ya kiafya kwa muda.

Mwezi Desemba 2024, alilazwa katika Hospitali ya Nakasero jijini Kampala kwa siku 11 kutokana na matatizo ya kongosho.

Baadaye, alisafirishwa kwenda Hospitali ya Allina Health Mercy nchini Marekani kwa matibabu zaidi, safari iliyogharamiwa na serikali ya Uganda chini ya Rais Yoweri Museveni.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa baba yake, Gerald Mayanja, Chameleone alizidiwa na kukimbizwa hospitalini Massachusetts baada ya kuzimia asubuhi ya Jumanne, Februari 18, 2025.

Rafiki yake, Juliet Zawedde, alithibitisha kuwa msanii huyo anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa mapafu na kongosho.

Zawedde aliandika kwenye mitandao ya kijamii: “Rafiki yangu kipenzi hajisikii vizuri leo. Amepelekwa hospitalini. Naomba kwa ajili yako, rafiki yangu mpendwa Chameleone. Najua kwa sasa hujisikii vizuri. Bwana akupe mguso wa uponyaji, arejeshe afya na nguvu zako, akufariji katika maumivu yako, na akupe ujasiri wa kukabiliana na changamoto hii.”

Familia na mashabiki wa Chameleone wanaendelea kumuombea apate nafuu haraka. Baba yake alieleza: “Chameleone alipaswa kufanyiwa upasuaji mapema, lakini uliahirishwa ili madaktari wafanye vipimo kuhakikisha mwili wake uko tayari kwa upasuaji. Walichunguza moyo wake, shinikizo la damu, macho, na aina ya damu kabla ya kuendelea, kama taratibu zinavyotaka.”

Kwa sasa, mashabiki na wapendwa wa Chameleone wanasubiri taarifa zaidi kuhusu maendeleo yake, wakitumaini atapona na kurejea kwenye jukwaa la muziki hivi karibuni.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Published

on

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”

Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.

Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.

Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.

Continue Reading

Entertainment

Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Published

on

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.

“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.

“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”

Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.

“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.

Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.

“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.

Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;

Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”

Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule 😁.”

D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya 🇰🇪.”

Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”

Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”

Continue Reading

Trending