Connect with us

Business

Bei ya vitunguu katika masoko ya humu nchini kuongezeka

Published

on

Bei ya Vitunguu katika masoko ya humu nchini huenda ikaongezeka hata zaidi kufuatia uhaba wa bidhaa hiyo.

Kufuatia hatua hiyo wafanyibiashara wa vitunguu humu nchini wamelazimika kuagiza bidhaa hiyo kutoka taifa jirani la Tanzania kufuatia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.

Wakizungumza na vyombo vya habari, Wafanyibiashara hao walisema kuna uhaba mkubwa wa vitunguu jambo ambalo limefanya bei kupanda.

Kulingana na wakulima wa zao hilo, hawakupanda vitunguu kutakana na gharama ya juu ya mbegu pamoja na  changamoto za mabadiliko ya hali ya anga.

Aidha walisema kuwa gharama ya Kilimo cha vitunguu imekuwa juu ikilinganishwa na mapato ya chini na ukosefu wa bei nzuri sokoni.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KEMFRI kuanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki

Published

on

By

Taasisi ya utafiti wa bahari na uvuvi nchini, KEMFRI, imeanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki, ili kuongeza upatikanaji wao na kuinua sekta ya uvuvi nchini.

Akizungumza jijini Mombasa, kaimu mkurugenzi mkuu wa KEMFRI, Dkt. James Mwaluma, alisema kuwa mradi huo unatekelezwa katika eneo la Shimoni kaunti ya Kwale na unalenga kuzalisha samaki wa thamani kubwa kama vile kamba, matiko, na aina nyingine ambazo upatikanaji wake ni nadra.

Dkt. Mwaluma alisema kuwa mbegu zitakazozalishwa kupitia mradi huo zitasambazwa kwa vikundi vya vijana na wanawake wanaojihusisha na shughuli za ufugaji wa samaki, ili kuwawezesha kujitegemea kiuchumi.

Aidha, aliwahimiza vijana kote nchini wakumbatie fursa zilizopo kwenye uchumi wa baharini akisema ni njia mojawapo ya kujikwamua kimaisha na kupambana na ukosefu wa ajira.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Kaunti ya Kilifi yaendeleza mikakati ya kuimarisha sekta ya uvuvi

Published

on

By

Mkurugenzi wa masuala ya uvuvi kaunti ya Kilifi Mwangi Gachuru amesema serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mikakati katika kuimarisha sekta ya uvuvi kwenye kaunti hii ya Kilifi.

Gachuru alisema wanashirikiana na wasimamizi wa fuo za bahari katika kaunti ya Kilifi katika kuhakikisha wavuvi wananufaika kupitia raslimali za baharini.

Aidha, Gachuru aliwahimiza wavuvi na wenyeji wa kaunti ya Kilifi kushirikiana ipasavyo kuhakikisha raslimali hizo zinawafaidi ipasavyo.

“Ni kupitia ushirikiano pekee ndipo mtaweza kuendeleza uvuvi wenu vizuri’’, alisema Gachuru

Akizungumzia mzozo baina ya wavuvi, Gachuru aliwataka kuzingatia sheria zilizopo kwa mujibu wa sheria za uvuvi ili kupatikane mwafaka na sio kuchukua sheria mkononi na kuahidi kuwa watawakabili kisheria wale ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku kutumika baharini kuvua samaki.

“Panapotokea ugomvi miongoni mwenu, zingatieni sheria na sio kuchukua sheria mkononi’’ Aliongeza Gichuru.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending