Connect with us

Business

Bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa yapanda

Published

on

Huenda wakenya wakagharamika zaidi katika kumudu gharama ya maisha kutokana na ongezeko la bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa mtawalia.

Hii ni kutokana na bei mpya iliyotolewa na Mamlaka ya kudhibiti Kawi na mafuta ya Petroli nchini EPRA kwani bei ya mafuta ya Petroli imeongezeka kwa shilingi 8.99, mafuta ya Dizeli kwa shilingi 8.67 na mafuta ya taa kwa shilingi 9.55 kwa lita.

Kulingana na EPRA, bei hiyo mpya itatumika kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi Agosti 14, ambapo bei ya mafuta ya Petroli katika jiji la Nairobi itauzwa kwa shilingi 186.31, Diseli kwa shilingi 171.58 na mafuta ya taa kwa shilingi 156.58.

Katika jiji la Mombasa bei hiyo mpya ya mafuta itauzwa kwa shilingi 183.02, mafuta ya Dizeli yatauzwa kwa shilingi 168.30 na mafuta ya taa yatauzwa kwa shilingi 153.29 kwa lita katika kipindi cha siku 30.

Hata hivyo katika kaunti ya Kilifi bei hiyo ya mafuta iko tafauti kwa sasa mafuta ya Petroli yatauzwa kwa shilingi 183.88, mafuta ya Dizeli yakiuzwa kwa shilingi 169.16 na matufa ya taa yatauzwa kwa shilingi 153.29 kwa lita.

Kulingana na taarifa kutoka EPRA, bei hiyo mpya mafuta imetoka na kupanda kwa bei ya mali ghafi kwa asilimia 6.45 ambayo ni Dola za Marekani 590.24 kwa “Cubic metre” kwenye mafuta ya Petroli mwezi Mei mwaka huu.

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka hiyo Daniel Bargoria alisema japo bei hiyo huenda ikashuka iwapo soko huru la mafuta litapunguza bei ya mali ghafi ambayo imechangiwa na mizozo ya kivita katika mataifa yanayopigana ambayo na yamekuwa yanazalisha mafuta.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Bei ya vitunguu katika masoko ya humu nchini kuongezeka

Published

on

By

Bei ya Vitunguu katika masoko ya humu nchini huenda ikaongezeka hata zaidi kufuatia uhaba wa bidhaa hiyo.

Kufuatia hatua hiyo wafanyibiashara wa vitunguu humu nchini wamelazimika kuagiza bidhaa hiyo kutoka taifa jirani la Tanzania kufuatia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.

Wakizungumza na vyombo vya habari, Wafanyibiashara hao walisema kuna uhaba mkubwa wa vitunguu jambo ambalo limefanya bei kupanda.

Kulingana na wakulima wa zao hilo, hawakupanda vitunguu kutakana na gharama ya juu ya mbegu pamoja na  changamoto za mabadiliko ya hali ya anga.

Aidha walisema kuwa gharama ya Kilimo cha vitunguu imekuwa juu ikilinganishwa na mapato ya chini na ukosefu wa bei nzuri sokoni.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

KEMFRI kuanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki

Published

on

By

Taasisi ya utafiti wa bahari na uvuvi nchini, KEMFRI, imeanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki, ili kuongeza upatikanaji wao na kuinua sekta ya uvuvi nchini.

Akizungumza jijini Mombasa, kaimu mkurugenzi mkuu wa KEMFRI, Dkt. James Mwaluma, alisema kuwa mradi huo unatekelezwa katika eneo la Shimoni kaunti ya Kwale na unalenga kuzalisha samaki wa thamani kubwa kama vile kamba, matiko, na aina nyingine ambazo upatikanaji wake ni nadra.

Dkt. Mwaluma alisema kuwa mbegu zitakazozalishwa kupitia mradi huo zitasambazwa kwa vikundi vya vijana na wanawake wanaojihusisha na shughuli za ufugaji wa samaki, ili kuwawezesha kujitegemea kiuchumi.

Aidha, aliwahimiza vijana kote nchini wakumbatie fursa zilizopo kwenye uchumi wa baharini akisema ni njia mojawapo ya kujikwamua kimaisha na kupambana na ukosefu wa ajira.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending