Connect with us

Entertainment

Baada ya Harusi ya Kai, Beka na Shanniez; Je, Inayofuata ni ya Kassim na Umazi?

Wapi unaweza kumpata mwenza wa maisha? Jibu linaweza kuwa popote—kanisani, mitandaoni, au kwenye safari za kawaida. Lakini kwa Kassim Mbui na Binti Umazi, jibu linaonekana kuwa wazi: sehemu ya kazi. Picha za wawili hao kutoka COCO FM ambazo zimenifikia huenda zikakushangaza kidogo ila ndio hivyo mapenzi hayatabiriki. Muda, kama kawaida, utatufunulia ukweli.

Published

on

Mara nyingi huulizwa, “Wapi mtu anaweza kumpata mwenza wa maisha?” Na mara nyingi, hakuna jibu moja sahihi. Wengine huwapata wake au waume zao kanisani, mitandaoni, au hata kwenye safari za kawaida na kwenye maeneo mengi mengine. Lakini ukweli ni kwamba sehemu ya kazi nayo si ya kubezwa. Hapo ndipo penzi linaweza kuchipua bila kutarajiwa.

Kwa watu kama Kassim Mbui na Binti Umazi, swali hilo linaweza kuwa na jibu moja: mahali pa kazi. Hawa wawili, ambao kwa sasa wanaendesha kipindi maarufu cha Janjaruka 254 ndani ya COCO FM, wamekuwa kivutio kikubwa si tu kwa uwezo wao wa kuwasiliana, bali pia kwa “chemistry” yao ya hewani na huenda of air pia.

Picha Zinasema Zaidi ya Maneno

Hali imezidi kuchanganya baada ya picha za wawili hao kunifikia. Katika picha hizo, Kassim anaonekana akiwa amepiga goti mbele ya Binti, huku Binti Umazi akiwa amevalia ‘gauni’ jekundu la kuvutia—rangi inayojulikana kwa kuwakilisha mapenzi. Katika picha hiyo, Binti anaonekana kustaajabu, kuishiwa na nguvu karibu kuanguka, kana kwamba amezidiwa na hisia.

Je, hilo lilikuwa ombi rasmi la uchumba? Au ni sehemu ya mradi wa kisanii ama kampeni ya matangazo? Bila shaka msomaji wangu unayefuatilia COCO FM kwa utapata jibu kwenye hili.

Chemistry ya Kazi au Zaidi ya Hapo?

Kassim na Binti wamekuwa wakituletea kipindi cha Janjaruka 254 kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja sasa, na kwa muda huo mfupi wameweza kuunganisha mashabiki na kuwapa burudani ya kipekee. Kipindi hicho hurushwa hewani kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa asubuhi ya saa nne hadi saa saba mchana, kupitia COCO FM, na kimejizolea mashabiki waaminifu wanaosubiri kusikia sauti zao kila siku.

Tusubiri Muda Uongee

Kama ilivyo kawaida yangu mimi huwa najipa kuamini sana MUDA. Kwenye swala hili, muda utakuwa mfunua ukweli. Kwa sasa, mashabiki wanaweza tu kuendelea kutazama, kusubiri, na kubashiri. Je, ni uchumba wa kweli au ni mbinu ya kisanaa? Bila shaka, ukweli utadhihirika muda si mrefu.

🔁 Je, una maoni au unadhani kweli mapenzi yamechipuka COCO FM? Niandikie kwenye comment!

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Afrikana

Published

on

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.

“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.

“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”

Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.

“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.

Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.

“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.

Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;

Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”

Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule 😁.”

D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya 🇰🇪.”

Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”

Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”

Continue Reading

Entertainment

Chris Brown Akanusha Shtaka la Kumshambulia Producer kwa Chupa

Published

on

Msanii nyota wa Marekani, Chris Brown, amekana mashtaka mawili mahakamani yanayohusiana na madai ya shambulio kwa kutumia chupa katika kilabu cha usiku jijini London miaka miwili iliyopita.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 anatuhumiwa kumsababishia mtayarishaji wa muziki majeraha ya mwili katika tukio ambalo waendesha mashtaka wamelieleza kuwa “halikuwa na uchochezi wowote”.

Pia anakabiliwa na shtaka la kumiliki silaha hatari — ambayo ni chupa ya kileo.

Mashtaka haya mawili yaliongezwa mwezi uliopita kwenye shtaka la awali, kubwa zaidi, la kujaribu kumsababishia mtu majeraha mabaya ya mwili (GBH), ambalo tayari Bwana Brown alilishatupilia mbali kwa kujitetea kuwa si kweli.

Chris Brown anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kesi hiyo mwezi Oktoba mwaka 2026.

Waendesha mashtaka wamesema kuwa mhanga wa tukio hilo, Abraham Diaw, alikuwa amesimama kwenye baa ya kilabu cha usiku kilichopo eneo la Soho mnamo tarehe 19 Februari 2023, wakati Chris Brown alimpiga kwa chupa mara kadhaa.

Mwimbaji huyo alikamatwa mwezi Mei katika hoteli ya nyota tano iliyopo Salford, Greater Manchester, baada ya kurejea Uingereza kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya muziki barani Ulaya.

Alizuiliwa korokoroni kwa takriban wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa dhamana baada ya kukubali kulipa ada ya dhamana ya pauni milioni tano (£5m) kwa mahakama.

Ada ya dhamana ni kiasi cha fedha kinachowekwa kama dhamana ya kifedha kuhakikisha mtuhumiwa atarudi mahakamani kwa kesi yake. Brown anaweza kupoteza fedha hizo endapo atakiuka masharti ya dhamana, ambayo yaliendelezwa katika kikao cha mahakama siku ya Ijumaa.

Kwa mujibu wa masharti hayo, Chris Brown anatakiwa kuishi katika anwani iliyopo Uingereza akisubiri kesi hiyo, na aliamriwa kukabidhi pasipoti yake kwa polisi.

Hata hivyo, ameruhusiwa kuendelea na ratiba ya ziara yake ya kimataifa ya Breezy Bowl XX kwa masharti kwamba atakabidhi pasipoti kila anapomaliza safari, na kuirudishiwa anapohitaji kusafiri kwa ajili ya maonesho.

Katika wiki za hivi karibuni, Brown amekuwa akitumbuiza kwenye viwanja na kumbi mbalimbali za burudani kote Uingereza na Ulaya, na kumaliza burudani mjini Paris mwishoni mwa wiki iliyopita. Sehemu ya ziara hiyo inayofanyika Marekani Kaskazini inatarajiwa kuanza baadaye mwezi huu na kufikia tamati tarehe 18 Oktoba.

Kikao kingine cha mahakama kimepangwa kufanyika tarehe 24 Oktoba.

Chris Brown ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa zaidi wa R&B nchini Marekani, akiwa mshindi wa tuzo mbili za Grammy na nyimbo 19 zilizofika katika nafasi 10 za juu kwenye chati za Uingereza, zikiwemo Turn Up The Music, Freaky Friday, With You na Don’t Wake Me Up.

Mshitakiwa mwenza, Omololu Akinlolu, raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 anayefahamika kisanii kama HoodyBaby, naye pia alikana shtaka la kumsababishia mtu majeraha ya mwili. Awali, alikana pia shtaka la kujaribu kusababisha majeraha mabaya ya mwili.

Chanzo: BBC

Continue Reading

Trending