Business
Ali Mbogo Aitaka Pwani Kuwawezesha Vijana Kunufaika na Uchumi wa Baharini

Serikali za kaunti za pwani zimetakiwa kuwawezesha vijana katika masuala ya ubaharia ili kujiendeleza kiuchumi.
Aliyekuwa mbunge wa Kisauni, Ali Mbogo, amesema kuwa ukosefu wa mikakati mwafaka kutoka kwa viongozi kuwawezesha vijana umechangia vijana wengi kukosa vibali muhimu vinavyohitajika ili kuajiriwa katika sekta hiyo ya uchumi wa baharini.
Mbogo ameeleza kuwa Pwani iko na fursa nyingi za kiuchumi kupitia bahari, na ni jambo la kusikitisha kuona vijana wakiachwa nyuma kwa kukosa mafunzo na vyeti vinavyotambulika kimataifa ili kuwawezesha kunufaika na ajira hizo.
Wakati uo huo mwenyekiti huyo wa bodi ya bandari ya LAPSSET amewahimiza vijana ambao hawakubahatika kuendelea na masomo, kujiunga na vyuo vya ufundi ili wapate ujuzi wa kazi za mkono na vyeti vitakavyowawezesha kupata ajira.
“Kuna nafasi nyingi sana katika bandari ya Mombasa lakini tuliowachangua hawatujali bali kujijali wenyewe.”
Business
Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.
Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.
Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.
Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.
Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .
Business
Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.
Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.
Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.
Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.