Connect with us

News

Matokeo Yataanza Kuja Tu

Published

on

Mkufunzi wa kilabu ya kiifi united Samson Jumbe amesema kwamba ana Imani vijana wake watarejea katika hali ya kupata matokeo chanya licha ya vijana wake kupoteza mechi 2 mfululizo ikiwemo debi kati yao na kilabu ya United Brothers mwishoni mwa jumwa

Kwa mujibu wa mwalimu huyo kwa sasa wanalenga kuimarisha safu yao ya mashambulizi ambayo imekua ikipoteza nafasi nyingi za wazi.

“Naamini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu vijana wangu wataanza kufunga magoli na kuanza kushinda mechi za ligi ya kaunti kuanzia wikendi hii nyumbani,mechi ya tumecheza vizuri kasoro magoli tu.”

Kwa upande wake kocha wa kilabu ya united Brothers Titus Kitaka amesema kwamba mazoezi mazito ambayo amekua na vijana wake imewasaidia pakubwa kupata matokeo mazuri tangu ligi hiyo kungoa nanga.

“Sisi ni ushindi tu kwa sababu tufanye mazoezi ya kutosha kwa ajili ya ligi hii ya kaunti na malengo yetu yanasalia pale pale kushinda na kupanda msimu ujao.”

Kilifi United inaketi nafasi ya 9 na imepoteza mechi mbili mfululizo kati nne ambazo wamecheza huku United Brothers wakishinda tatu na kupoteza moja pekee.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.