Connect with us

News

Kenya Police Bullets Mabingwa KWPL

Published

on

Kilabu ya akina dada Kenya Police Bullets ndiyo mabingwa wa ligi ya taifa akina dada kwpl baada ya kuwanyuka Trinity starlets magoli 4-0 mechi ya mwisho hapo jana ugani afraha stadium Nakuru

Winga matata Emily Kemunto moranga alifungua ukurasa wa magoli dkaika 40,kisha Mshambulizi matata Rebecca Becky Okwaro akifunga magoli matatu dakika ya 55 ,dakika ya 79 na dakika 89 na kuchukua kiatu cha dhahabu kwa kufunga magoli 16 msimu huu

Kocha wa Bullets Beldine Odemba hakuficha furaha yake baada ya kushinda kombe hilo kwa mwaka wa pili mfululizo akitaja kwamba upinzani ulikua mkali ila wasichana wake wamepigana mpaka siku ya mwisho kubeba taji hilo.

Katika matokeo mengine

Kisped Queens 2-1 Vihiga Queens

Bunyore Starltes 0-3 Bungoma Queens

Kibera soccer Women  7-0 Mombasa olympic

Ulinzi Starlets 4-0 Kisumu All Starlets

JEDWALI

Bullets alama 46

Ulinzi starlets 45

Kibera soccer alama 42

Kayole starlets ni mabingwa wa KWNSL Baada ya kunyuka kayolets 3-0 madira soccer assasin

Iron ladies 3-0 Diani Quens na kushinda taji la fkf divisheni ya kwanza.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto Awaomba Radhi Watanzania.

Published

on

By

Rais William Ruto amejitokeza na kuomba msamaha kwa niaba ya vijana wa Gen Z dhidi ya utawala wa Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Rais Ruto ameisihi serikali ya Tanzania kuondoa hofu kuhusu Mabishano makali ya Mtandaoni baina ya mataifa  haya mawili  licha ya Viongozi wa mataifa haya mawili Rais William Ruto na Mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  kuonekana kujaribu kuuzima moto wa mashambulio ya mitandaoni hasa miongoni mwa vijana wa Gen Z.

Akizungumza wakati wa dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa yaliondaliwa jijini Nairobi, Rais Ruto amesema kuna haja ya kuendeleza ushirikiano mwema wa kidiplomasia na wala sio kuchangia uhasama, akiwaomba msamaha pia vijana wakenya.

Viongozi wahudhuria dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa

Kauli ya Rais Ruto imejiri baada Bunge la Tanzania kulazimika  kusitisha vikao vya kawaida na kujadili hoja inayotajwa kugusia usalama wa taifa la Tanzania huku wakimpongeza rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua aliyochukua ya kuwafurusha Wanaharakati  wa kutetea haki za binadamu wakiongozwa na Martha Karua ambaye kiongozi wa chama cha People’s Liberation Party nchini Kenya na Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga, Mwanaharakati Boniface Mwangi wa Kenya na Agather Atuhaire wa Uganda.

Mwanaharakati Bonifance Mwangi alipatikana  katika eneo la mpakani mwaka Kenya na Tanzania katika eneo la Lunga lunga ilihali mwenzake  Agather Atuhaire akipatikana karibu na kituo cha mpakani na Mtukula.

Continue Reading

News

Manusua wa Mkasa Baharini, Kilifi

Published

on

By

Mafisa wa uokoaji kaunti ya Kilifi bado wanaendelea kupiga mbizi baharini kutafuta Mwili wa Mwanabaharia mmoja Kapteni Kivondi, aliyezama Jumamosi usiki wa tarehe 24 Aprili, akiwa na wengine wawili katika mkono wa Bahari mjini Kilifi.

Kapteni Kivondi alifariki pamoja na mwenzake Kapteni Mwidini wakati wa mkasa huo, huku baharia mwengine wa tatu Aisha Jumwa akinusurika baada ya kuogelea baharini kwa zaidi ya masaa 16.

Akizungumza na CocoFm iliyomtembelea Hospitalini mjini Kilifi, Jumwa alielezea matukio hayo wakati mawimbi makali yalipopiga chombo chao na kukizamisha.

Mwili wa baharia mwengine ambaye alikuwa msaidizi wa nahodha wa Dau hilo, Kapteni Mwidini ulipatikana katika ufuo wa Watamu, umbali wa kilomita 50 kutoka mji wa Kilifi. Mwili wa marehemu uliondolewa na kusafirishwa hadi eneo la Likoni Mjini Mombasa kwa Maziko.

Aisha Jumwa -Manusuru wa mkasa wa baharini mjini Kilifi

Jumwa anasema kuwa aliweza kuokolewa siku iliyofuatia ya Jumapili, mwendo was saa sita adhuhuri baada ya kuogelea kwa maasaa hayo 16 licha ya upepo na mawimbi makali yaliyozidi kumsukuma maji makuu.

Kisa hiki kilitokea masaa machache tu hata baada ya idara ya Utabiri wa hali ya hewa kutoa tahadhari ya kuchafuka kwa Bahari na marufuku ya kuepuka fuo za bahari.

Hata hivyo Jumwa anasema kuwa tahadhari hiyo iliwapata kuchelewa hadi mkasa huo ulipowakuta. Anaongeza kwamba baada ya Dau lao kuzama watatu hao walijifunga Kamba ili waweza kuolea na kusaidiana lakini wawili hao wakashindwa na nguvu ya mawimbi hayo makali na kuaga dunia mikononi mwake

Taarifa ya Lolani Kalu

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.