Connect with us

News

Matokeo Yataanza Kuja Tu

Published

on

Mkufunzi wa kilabu ya kiifi united Samson Jumbe amesema kwamba ana Imani vijana wake watarejea katika hali ya kupata matokeo chanya licha ya vijana wake kupoteza mechi 2 mfululizo ikiwemo debi kati yao na kilabu ya United Brothers mwishoni mwa jumwa

Kwa mujibu wa mwalimu huyo kwa sasa wanalenga kuimarisha safu yao ya mashambulizi ambayo imekua ikipoteza nafasi nyingi za wazi.

“Naamini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu vijana wangu wataanza kufunga magoli na kuanza kushinda mechi za ligi ya kaunti kuanzia wikendi hii nyumbani,mechi ya tumecheza vizuri kasoro magoli tu.”

Kwa upande wake kocha wa kilabu ya united Brothers Titus Kitaka amesema kwamba mazoezi mazito ambayo amekua na vijana wake imewasaidia pakubwa kupata matokeo mazuri tangu ligi hiyo kungoa nanga.

“Sisi ni ushindi tu kwa sababu tufanye mazoezi ya kutosha kwa ajili ya ligi hii ya kaunti na malengo yetu yanasalia pale pale kushinda na kupanda msimu ujao.”

Kilifi United inaketi nafasi ya 9 na imepoteza mechi mbili mfululizo kati nne ambazo wamecheza huku United Brothers wakishinda tatu na kupoteza moja pekee.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

News

Amref, yaikabidhi kaunti ya Kilifi vifaa ya matibabu vya milioni 13.2

Published

on

By

Shirika la Afya la AMREF kwa ushirikiano na serikali ya kaunti ya Kilifi wawekeza zaidi katika sekta ya afya ili kukabiliana na magonjwa yaliyosaulika.

Shirika hilo limeikabidhi serikali ya kaunti ya Kilifi vifaa vya matibabu vya thamani ya shilingi milioni 13.2 ili kuwawezesha wahudumu wa afya kutathmini magonjwa mbalimbali yaliyosaulika na kuboresha sekta ya afya mashinani.

Mkurugenzi wa Shirika la Afya la AMREF humu nchini Daktari Ndirangu Wanjuki, amesema vifaa hivyo vitasaidia katika kubaini magonjwa yaliyosaulika kama vile Kichocho na kuwawezesha wahudumu wa afya kuwahuhudumia wagonjwa ipasavyo.

Akizungumza wakati wa halfa ya kupokea vifaa hiyo katika hospitali kuu ya rufaa ya Kilifi, Gavana wa kaunti Kilifi Gedion Mung’aro amesema vifaa hiyo vitasambazwa katika hospitali na zahanati 15 za kaunti hiyo.

Gavana Mung’aro amesema magonjwa kama vile Kichocho na Matende miongoni mwa wagonjwa mengine yatagunduliwa kwa urahisi na kutibiwa kwani mengi husababishwa na viini kwenye maji machafu hasa kandokando ya mito.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.