News
Kadinali Farrell: Papa Francis Atazikwa Jumamosi Aprili 26

Uongozi wa Kanisa Katoliki mjini Vatican umetangaza kwamba Papa Francis atazikwa siku ya Jumamosi Aprili 26 katika Kanisa kuu la mtakatifu Bikiri Maria mkuu kuanzia mwendo wa saa nne asubuhi kwa kuambatana na Ibada ya Misa.
Kulingana na Kadinali Kevin Farrell, Camerlengo wa baraza la kitume la Kanisa Katoliki, uamuzi huo umeafikiwa kufuatia mkutano wa makadinali wote waliowasili Vatican kwa mipingo na maadilinzi ya mazishi kabla ya waumini wa Kanisa Katoliki kuruhusiwa kuutazama mwili wa Papa.
Kadinali Farrell amesema kwa kuzingatia kanuni na desturi za Kanisa Katoliki baada ya Papa kuaga dunia, Kanisa limefunga makaazi ya Papa kwa kitambaa chekundu kuashiria kwamba Papa amefariki na mwili wake umewekwa ndani ya jeneza katika Kanisa la Casa Santa Marta mjini Vatican huku maombi maalum yakiendelea.
Kulingana na desturi za Kanisa Katoliki baada ya mazishi makadinali watakusanyika pamoja katika chumba maalamu yaani Conclave ili kuanza mchakato wa kumchagua Papa mpya katika kipindi cha siku 15 hadi 20 na mchakato huo umepangwa kuanza rasmi mwezi Mei tarehe 5.
Pete ya Papa Francis, pia huvunjwa na kuharibiwa ishara ya ukomo wa maisha yake ya Papa.
Itakumbukwa kwamba Papa Francis aliaga dunia mnamo siku ya Jumatatu Aprili 21 mwendo wa saa moja na nusu asubuhi baada ya kuugua dunia akiwa na umri wa miaka 88.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.
News
Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.
Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.
Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.
Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.
Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.