Connect with us

Health

Vilabu Vya Burudani Kufungwa Malindi Kisa Mziki wa Sauti ya Juu

Published

on

Photo: Courtesy

Idara ya mazingira katika kaunti ya Kilifi imeanzisha mchakato wa kuvifunga vilabu na maeneo ya burudani mjini Malindi ambayo yamekuwa na tabia ya kuchezesha mziki wa sauti ya juu nyakati za usiku.

Akizungumza na Wanahabari mjini Malindi, Afisa mkuu wa idara ya mazingira kaunti ya Kilifi Zamzam Ali amesema vilabu hivyo vya burudani vimekuwa vikikiuka sheria za Mazingira hasa maeneo yalio karibu na vituo vya afya na shule.

Ali amedokeza kwamba hatua hiyo itakuwa funzo kwa watu na maeneo mengine kaunti ya Kilifi ambayo yamekuwa na tabia ya kutatiza wananchi kwa uharibifu wa Mazingira.

Kwa upande wao wamiliki wa mahoteli mjini Malindi wakiongozwa na Nicholus Ranford wameelezea kutoridhishwa na uharibifu wa mazingira huku wakiitaja tabia ya vilabu vya burudani kucheza mziki kwa sauti ya juu hasa nyakati za usiku ni kero kwa watalii.

Haya yamejiri baada ya baadhi ya vilabu vya burudani mjini Malindi kaunti ya Kilifi kuonekana kukiuka sheria za mazingira kwa kuendeleza sherehe zao kwa kucheza mziki kwa sauti ya juu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.