Business

Wafugaji wa Kuku Jilore Wataka Mafunzo ya Kisasa Kutokomeza Hasara

Published

on

Wafugaji wa kuku katika eneo la Jilore kaunti ya Kilifi wameitaka serikali ya kaunti kuwapa mafunzo ya kisasa kuwawezesha kuendeleza ufugaji ili kuepuka hasara ambazo wamekuwa wakishuhudia mara kwa mara.

Kulingana na Ishmael Menza wafugaji wengi hawana ufahamu kuhusu mbinu za kisasa za ufugaji hali ambayo inasababisha mapato duni.

Akizungumza na Coco FM, Menza anasema kuwa wafugaji hasa wadogo wamekuwa wakikadiria hasara kufuatia magonjwa yanashambulia kuku akisema wengi hajui aina za dawa ambazo wangetumia.

Hata hivyo Menza aimeitaka serikali kupunguza bei za dawa na chakula ili kuwasaidia wakulima hao wadogo kuendeza ufugaji bila changamoto.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version