Connect with us

Sports

Cherotich Na Yavi Kuzindua Uhasama Tena,Oregon

Published

on

Bingwa wa nishani ya fedha mbio za olimpiki mitaa 3000 kuruka maji na viunzi Faith Cherotich anatarajiwa tena kuzindua uhasama na bingwa wa Olimpiki raia wa Bahrain Winfried Yavi na Mganda Peruth Chemutai katika msururu wa Prefontaine Classic Diamond League kule Eugene, Oregon Marekani hapo kesho.

Raia huyo anaingia kwenye mbio hizo akiwa na mortisha ya hali ya juu baada ya kushinda Yavi katika misururu mitatu msimu huu mbio za Doha nchini Qatar,Oslo kule Norway na Brussels.

Cherotich akiwa tayari amekusanya alama 24 dhidi ya 14 ya Yavi kuelekea katika msururu mwingine mjini Monaco Ufaransa Julai 11.

Msimamo wa 2025 Wanda Diamond League – Women’s 3000m hadi sasa;
Faith Cherotich (KEN) – 24 pts

Winfred Yavi (BRN) – 14 pts

Sembo Almayew (ETH) – 12 pts

Maraw Bouzayani (TUN) – 10 pts

Peruth Chemutai (UGA) – 9 pts

Lea Meyer (GER) – 8 pts

Courtney Wayment (USA) – 7 pts

Gabrielle Jennings (USA) – 6 pts

Norah Jeruto (KAZ) – 5 pts

Lomi Muleta (ETH) – 4 pts

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.   

Published

on

By

Huku zikiwa zimesalia siku 15 pekee kung’oa nanga kwa kipute cha CHAN mwezi ujao,
Kenya imeratibiwa kupambana na DRC, Morocco, na Angola katika Kundi A linalotajwa kuwa ndio kundi gumu zaidi yaani Kundi la Kifo.
KUNDI B
Ni Taifa jirani la Tanzania, Burkina Faso, Madagascar na Jamhuri ya Africa ya Kati.
KUNDI C
Uganda itachuana na Algeria,Africa Kusini,Guinea na Nigeria.
KUNDI D:
Congo itakabana koo na Nigeria,Senegal na Sudan Kusini.
 Mechi hizi zitasakatwa katika nyuga za katika Kenya, Uganda na Tanzania,
Continue Reading

Sports

Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Published

on

By

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.

Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.

Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.

Continue Reading

Trending