News
Boniface Mwangi akamatwa na maafisa wa DCI
Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu nchini Boniface Mwangi amekamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI.
Kulingana na Mkewe Boniface, Hellen Njeri Mwangi, Mumewe amekamatwa nyumbani wako katika eneo la Lukenya kaunti ya Machokos na maafisa waliojitambulisha kwamba wanatoka katika Idara ya DCI.
Hellen alisema Boniface amepelekwa katika makao makuu ya idara ya DCI jijini Nairobi huku sababu za kukamatwa kwa Boniface zikihusisha na masuala ya ugaidi.
Kulingana na Wakili wa Boniface, James Kamau alisema maafisa wa DCI walivamia makaazi ya mteja wake wakiwa wamejihami kwa silaha na kumtia nguvuni.
Hatua hii imejiri baada ya Boniface na Mwanaharakati kutoka Uganda Agather Utuhaire mnamo siku ya Ijumaa Julai 18, 2025 kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Afrika Mashariki na kulishtaki taifa la Tanzania kwa madai kwamba maafisa wa serikali ya Tanzania walikiuka haki zao za kibinadamu.
Kwenye mashtaka hayo, Wanaharakati hao walidai kutekwa nyara na watu wasiojulikana wakiwa jijini Dar er Salam pamoja na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na kutupwa nje ya mpaka wa Tanzania, Uganda na Kenya, mtawalia.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi